Askari hao wa TANAPA walimaliza mafunzo
hayo hapo juzi kwenye chuo
hicho cha wanyama Pori
cha Mlele ikiwa ni mafunzo ya
kwanza hapa nchini
kwa TANAPA kutoa mafunzo kama hayo kwa Askari wa wanyama pori
kupatiwa mafunzo hayo kabla ya
kuanza kazi
Waliyataja baadhi
ya mafunzo waliyoyapata kuwa ni namna ya kufanya doria , kukamata wahalifu,
kumpekua mhalifu na kutotumia
nguvu sana katika kukamata mhalifu pia wamejifunza namna ya kutumia silaha.
Walieleza katika kipindi hicho cha mafunzo
wahitimu hao walifanikiwa kukamata wahalifu 50 wakati wakifanya
doria katika maeneo mbambali ya
Mbuga ya Katavi na kwenye mapori ya akiba ya Rukwa Lwafi
Wahitimu hao
walieleza kuwa mafunzo hayo
yaliwashirikisha Askari 99
lakini watatu kati yao
wameshindwa kuhitimu zikiwemo
sababu mbambali kama
utoro na utovu wa nidhamu hali ambayo ilfanya wahitimu waliomaliza kubaki 96 ambapo kati yao mwanamke ni mmoja
na wanaume ni 95
Kwa upande wake
mkuu wamapori ya akiba ya Rukwa Lwafi
Joseph Mbung’ombe alimweleza mkurugenzi mkuu wa TANAPA kuwa chuo hicho
kinakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Alizitaja
changamoto hizo kuwa ni ukosefu wa mawasiliano
na ubovu wa miundo mbinu ya barabaa na
upungufu wa magari pamoja
idadi ndogo ya washiriki wa
mafunzo kwa wanawake na ufinyu wa bajeti
Nae Mkurugenzi wa Hifadhi
na Ikolojia Martini Loibook alieleza kuwa mafunzo hayo walioyapata
yanaumuhimu sana hasa kutokana na changamoto zinazoikabili nchi yetu
inayokabiliwa na wimbi la ujangili
Pia Mkurugenzi
wa utumishi na utawalla
wa TANAPA Witnes Shoo aliwataka wahitimu hao kufanya kazi
kwa uaminifu kwa kujituma na
wawe na nidhamu na wasiwe na tabia ya kutoa siri za ofisi.
Mkurugenzi
Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi
aliwaasa wahitimu hao wahakikishe
wanafanya kazi zao kwa uaminifu
mkubwa hasa katika shughuli zao katika kupambana kukomesha ujangili.
Aliwataka
kutojihusisha na masuala ya ujangili na
badal awahakikishe wanafanya kazi za kupambana na mitandao ya ujangiri iliyopo
ndani ya nchi na nje ya nchi
Alisema wapo
baadhi ya watumishi wa TANAPA ambao wamekuwa sio waaminifu hivyo wahitimu hao
wahakikishe wanafanya kazi zao kwa uaminifu pasipo kurubuniwa na mtu yoyote
yule au watu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni