Jumatano, 23 Aprili 2014

MAKALA: UTALII WA FANI YA PICHA UIMARISHWE



Utalii,aghalabu, ni kuhusu kuona. Hivyo vya kuonja (utalii wa vyakula), kusikia (utalii wa kiutamaduni, hasa muziki) ni vitu vinavyokuja baadaye.
Moja ya changamoto zinazokabili sekta ya utalii ni utangazaji wa ndani na nje  Sekta hii kwa kweli ni muhimu sana katika maendeleo ya nchi, lakini mfumo wa utangazaji iliwateja waweze kujua vivutio vilivyoko bado haujaendelea sana.
Lakini mtalii, kimsingi  huja  kutaka kushuhudia mambo ambayo amesikia habari zake, au ameona kupitia matangazo, hasa ya picha (za mnato na za kujongea- video).
Wakati hilo ni muhimu  lakini matumizi ya video  na  picha  kuvutia  utalii  kwa  humu  ndani yako kwa kiwango cha chini sana.
Ngorongoro, kwa mfano, wengi tunaisikia kwa jina, uhamaji wa wanyama kule Serengeti, tunasikia kwa jina tu, lakini hakuna mfumo mzuri wa kipicha wa kuwaonyesha wananchi. Sababu kubwa ni kuwa vyombo vya habari nchini haviweki maeneo ya utalii kama sehemu muhimu ya habari zao na hivyo tuwe tunaoneshwa mara kwa mara.
Aidha vyombo vya habari haviweki ratiba ya kutembelea au kuwepo kwenye maeneo ya tukio- wanyama wanapohama, ili kuwaonesha wananchi nini kinatokea na hivyo kuwajengea hamasa ya wananchi nao kuwa katika eneo la tukio katika msimu mwingine.
Lakini kikwazo kikubwa ni kuwa nchi kwa ujumla haijaweka mkazo mkubwa wa kutumia picha kama moja ya njia ya kuweka kumbukumbu za kitaifa. Na kwa sababu hiyo mafunzo katika picha nchini – mfano kwenye vyuo vya uandishi wa habari na vyuo vikuu, hayafikiriwi kabisa, isipokuwa ni kama kwa ajili ya uandishi wa habari za magazeti na televisheni.
Lakini  somo  la  picha  katika  upana  wake    na  ukuzaji  utalii, hakuna mkazo kimafunzo. Juhudi zangu binafsi  pale Chuo  Kikuu  panatakiwa  kuwahamasisha  wafanyakazi  kuweka mafunzo  ya  picha  bado  zinagonga  mwamba  kwa  sababu  ya  kutoona umuhimu wake licha ya kuwa mtaala unaainisha uwepo wa kozi hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni