Jumatatu, 15 Desemba 2014

Mabadiliko makubwa Maliasili na Utalii



Mabadiliko makubwa Maliasili na Utalii
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/1596856/data/43/-/appotyz/-/ico_plus.png Rating
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2435150/highRes/666917/-/maxw/600/-/fwlbqt/-/nyalandu.jpg
Lazaro Nyalandu 


Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya wakurugenzi waliohusika katika uteuzi huo, zinaeleza kuwa mabadiliko hayo yalifanyika hivi karibuni na barua za kutekeleza majukumu yao mapya walipewa juzi

. Serikali imefanya mabadiliko makubwa ya wakurugenzi wanane wa Wizara ya Maliasili na Utalii akiwamo aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Wanyamapori, Paul Sarakikya ambaye amehamishiwa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (Tawiri).
 
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya wakurugenzi waliohusika katika uteuzi huo, zinaeleza kuwa mabadiliko hayo yalifanyika hivi karibuni na barua za kutekeleza majukumu yao mapya walipewa juzi.
Hata hivyo, Waziri wa wizara hiyo, Lazaro Nyalandu alipoulizwa kuhusu suala hilo alisema atalizungumzia Jumatatu ijayo.
Taarifa kutoka ndani ya wizara hiyo, zilieleza kwamba barua ya mabadiliko hayo imeandikwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Utumishi, George Yambesi.
Akizungumza na gazeti hili jana Yambesi alisema, “Taratibu za uteuzi wa wakurugenzi ndani ya wizara ziko wazi kwamba zinafanywa na katibu mkuu wa wizara hivyo (Maimuna Tarishi) hivyo naomba mtafuteni yeye.” Hata hivyo Tarishi hakuweza kupatikana kuzungumzia mabadiliko hayo.
Katika mabadiliko hayo, aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Wanyamapori, Profesa Alexander 

Songorwa amepelekwa kuwa Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Afrika, Mweka na mkurugenzi mpya ameteuliwa kuwa Herman Keraryo aliyekuwa mkurugenzi msaidizi wa idara hiyo.
Aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Matumizi Endelevu ya Wanyamapori, Profesa Jafari Kidegesho amepelekwa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (Sua).
Dk Charles Mulokozi aliyekuwa Kaimu Mkuu Msaidizi Matumizi Endelevu Wanyamapori anabaki katika nafasi hiyo na Julius Kidede amepelekwa Ngorongoro kupangiwa majukumu mengine ya kazi.
Mkuu wa Kitengo Kidogo cha Migogoro cha Wanyamapori ameteuliwa David Kanyata na Faustine Masalu akiteuliwa kuwa Mkurugenzi Uzuiaji Ujangili nchini, awali alikuwa Mkuu wa Kikosi cha Kuzuia Ujangili Kanda ya Mashariki- Dar es Salaam.

Kwa upande wake Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa akizungumzia mabadiliko hayo, alisema kubadilishwa kwa wakurugenzi hao ni jambo zuri lakini haliwezi kuleta ufanisi endapo Ikulu itaendelea kuingilia utendaji wa wizara hiyo.
“Bado watendaji wa juu wanaingilia utendaji kazi wa wizara, katika hotuba yangu bungeni nilipendekeza wakurugenzi hao kuchukuliwa hatua jambo ni jema, lakini bado wizara hii ina matatizo lukuki ambayo ili kuyamaliza kunahitajika kufanyika kwa ushirikiano wa wadau wote,” alisema Msigwa ambaye ni Mbunge wa Iringa Mjini kupitia Chadema.
Akizungumzia uteuzi huo, Keraryo alisema ameupokea kwa furaha na kuahidi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni zinavyomtaka kutenda.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni