Jumatano, 5 Agosti 2015

DKT.MERU: Moja ya kipaumbele chetu ni kuigeuza TTB kuwa Mamlaka


Dar es Salaam.

 Na mwandishi wetu.


Wizara ya Maliasili na Utalii imeahidi kuupa kipaumbele mchakato wa kuifanya Bodi ya utalii Tanzania (TTB) kuwa Mamlaka ya Utalii Tanzania (TTA) kwa lengo la kuiwezesha bodi hiyo kufanya kazi kwa ufanisi na kutekeleza majukumu yake kwa ukamilifu.Aidha Mamlaka hiyo imeitaka TTB kuangalia ni maeneo gani yanayoweza kuwa vyanzo vya mapato vitakavyoiwezesha bodi kupata fedha.
  Hayo yamesemwa na Katibu wa Maliasili na Utalii,Dkt.Adelhem Meru alipotembelea makao makuu ya Bodi ya  Utalii yaliyoko katika jengo la ISP  jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na wafanyakazi  wa bodi hiyo.
Dkt.Meru ameipongeza bodi ya utalii kwa kuendelea kufanya kazi  vizuri katika mazingira yenye changamoto  nyingi hasa za kifedha.Amesema TTB ndio chombo pekee chenye mamlaka ya kutangaza  vivutio vya utalii kwa ujumla wake , hivyo kinapaswa kuwezeshwa kutimiza jukumu hilo kwa niaba ya nchi  badala ya kila taasisi kutangaza vivutio inavyosimamia.
 Tunawajibika kwa kuwawezesha TTB mtekeleze majukumu yenu vizuri kwa kuwa ninyi ndio mliokabidhiwa jukumu la kutangaza vivutio vya utalii kama vile vya,fukwe,wanyama,historia  ,milima nk” alisema.
Hii ni ziara ya kwanza kwa Dkt.Meru kutembelea Makao Makuu ya Ofisi ya Bodi ya Utalii tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo,Bodi ya Utalii ni  moja ya taasisi zilizoko chini ya wizara yake yenye jukumu la kutanga vivutio vya utalii vya Tanzania ndani na nje ya nchi.

Mfanyakazi wa TTB Bw.Geofrey Tengeneza ambae ni Mkuu wa kitengo cha uhusiano akielezea jambo kwa Katibu Mkuu wa Maliasili  na Utalii (wa kwanza kushoto)Dkt.Adelhem Meru alipotembelea ofisi za bodi ya utalii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni